02/02/2026
KWANINI WAMPIGE MANGUNGU
Nina laani vikali sana kitendo cha kinyama, cha kiudhalilishaji na kisichokuwa cha kiungwana alichofanyiwa Leo Mwenyekiti wetu MURTAZA ALLY MANGUNGU na baadhi ya mashabiki wenzetu wa Simba, naliomba jeshi la .tanzania
Kuchukua Hatua za kisheria kwa wale watu wote ambao walihusika na kitendo hicho maana picha za video zipo zinawaonyesha sura zao ili iwe fundisho kwa mashabiki oya oya wengine k**a hao kukomesha kabisha upumbvu huu.
Mangungu sio kiongozi pekee yake ndani ya Simba Sasa kwanini timu ikifanya vibaya alaumiwe yeye pekee yake?
Mangungu hasajili yeye wachezaji, aliyetoa pasi ya goli Leo kwa mshambuliaji wa Timu pinzani Kisha ESPERANCE wakapata bao la kwanza ambalo liliwapa NGUVU ni Kante Sasa iweje ashambuliwe Mwenyekiti wetu?
AKILI za kuambiwa Changanya na za kwako mfumo wa Simba tulionao haumpi mamlaka ya MOJA kwa MOJA Mwenyekiti wetu wa Simba Sasa kwanini lawama apewe yeye?
Wachezaji wote unaowaona wanaosajiliwa Simba yeye hausiki Sasa kwanini timu ikifungwa alaumiwe yeye?
Mangungu yeye sio ambaye anatoa mishahara na posho kwa wachezaji timu ikifungwa Sasa analaumiwa yeye kwa kosa lipi?
NAOMBENI Wana Simba mtafakari tatizo la Simba kufanya vibaya lipo wapi na sio TU kuwashambuliwa watu ambao hawahusiki.