20/06/2021
Mlipokuwa mnazungumza kuhusu tiba za kiafrika, nikamkumbuka bwana mmoja wa kuitwa Imhotep.
_________
Leo hii ukiuliza nani baba wa tiba duniani 'father of medicine' utaambiwa ni Hippocrates kutoka ugiriki anayeaminika kuwa ndiye mwanzilishi wa sayansi ya tiba. Hippocrates alizaliwa na kupata kuishi miaka ya 460BC huko Kos, Ugiriki akifundisha na kuandika vitabu vingi kuhusiana na mambo ya tiba. Inaelezwa aliweza kuandika vitabu zaidi ya 60 ikiwemo kile cha "Hippocrates Oath" kinachoelezea kanuni na misingi ya maadili ya kazi za kitabibu. Kitabu hiko ndio chanzo wa kuwepo kwa kiapo cha madaktari na manesi.
Lakini, pamoja na Hippocrates kuitwa 'father of medicine', kuna mtu mwingine wa kuitwa Imhotep, mzaliwa wa Kemet au wengine wakiita Misri ya Kale. Huyu alikuwa mtaalamu wa mambo ya tiba pale Kemet akifundisha watu namna ya kutibu magonjwa na majeraha mbalimbali kwa kutumia vitu asili. Kuna wanasayansi wanasema kuwa Imhotep ndiye anayestahili kuitwa 'father of medicine' na sio Hippocrates. Hiyo ni kutokana na kugundulika kwa nyaraka iliyoandikwa miaka ya ~2500BC ikielezea maswala ya tiba. Hiyo inatoa tafsiri kwamba miaka 2000 kabla ya kuzaliwa Hippocrates, kulikuwa na nyaraka inazoelezea matibabu na magonjwa mbalimbali. Nyaraka hiyo iliyopewa jina la "Edwin Smith Papyrus" inasemekana iliandikwa na Imhotep.
Nyaraka hiyo iliyopatikana mwaka 1862, ilituthibitishia kwamba wamisri wa kale walikuwa wakitibu majeraha kwa kutumia asali na utomvu wa miti. Pia mafuta ya mnyonyo na baadhi ya matunda k**a vile 'mitini' (figs) yalikuwa ni dawa kwa maradhi mbalimbali ikiwemo maumivu ya mitupa. Mbogamboga k**a figili zilitumika kutibu maumivu ya viungo vya mwili. Majani ya Acacia nayo yalionekana kutibu kikohozi na hadi leo inatumika. Hayo yote yalielezwa na Imhotep kwenye maandiko yake. Imhotep, hakuwa tu mtaalamu wa tiba, bali alikuwa mtawala, katika serikali ya farao Djoser aliyetawala kuanzia mwaka 2960BC. Imhotep alikuwa mshauri wa farao, na kubwa kuliko vyote alikuwa ni msanifu majengo. Yeye ndiye aliyesanifu ujenzi wa piramidi ya kwanza nchini Misri iliyojulikana k**a piramidi ya ngazi 'step pyramid' iliyopo saqqara.
Imhotep alifariki miaka ya ~2950BC. Na kutokana na utaalamu wake katika maswala ya tiba, mwaka 525BC, wamisri na wagiriki walianza kumuabudu k**a mungu wa tiba.
_________
Ahsante.