17/05/2024
From EAGT wokovu ndiyo Sasa ministries center by ev kedmon nyawaje.
SOMO:NGUVU YA UPOTEVU IMEMWAGWA DUNIANI ILI KUWAPELEKA WENGI JEHANAMU. 2THESALONIKE 2:11---12.
Nataka nikwambie ewe mwana na mtu wa Mungu. Leo hii NGUVU kubwa IMEMWAGWA ya upotevu watu WENGI wanaelekea JEHANAM.hususani watu wa dini wanaenda jehanamu kwenye mateso hivi hivi.
KWANINI: watu hawasomi maandiko wakayatafakari Ili yawafundishe kuijua kweli ya YESU.ngoja nikuoneshe viashiria hivyo ambavyo vinaonesha jehanamu anachekelea kwa kuwapokea WENGI:Leo hii watu wanamichepuko wamama na wababa,ndoa za mitala,ulevi,ukahaba na kafara na Bado wanaenda kanisani ukiwashuhudia okoka utaambiwa Nina KANISA langu KANISA Gani hilo uchafu TU.
Mambo mengine kupoteza hamu ya ibada unaenda TU k**a desturi jehanamu inakuhusu,kupoteza kwa kiu ya kusoma neno mara kwa mara na maombi yaani wewe ni mkavu mkavu k**a gogo huwezi hata kuomba au kugunga wewe jehanamu yako,kukata tamaa ya kusonga mbele kutokana na shida za Dunia umeisha wewe humwamini Mungu kuwa anaweza,makanisa mengi ya uongo yataongezeka na mafundisho Yao ya uongo jehanamu yenu,watu wanakataa kuokoka yaani waache maovu na kumkabidhi YESU maisha Yao jehanamu inakuja.watu wako bize na mambo ya Dunia kuliko Mungu weeeee jehanamu inawaka moto.mmmh mtu yupo tayari kuamka usiku kwenda kuangalia mpira kwenye vibanda umiza lakini kupiga goti TU na kuomba hawezi hehehehe YESU akusaidie,mtu Yuko tayari kuhonga mchepuko lakini nyumbani au ndugu wanateseka aaah imekula kwako.hebu geuka Leo YESU akusaidie.ni Mimi mtumishi wa Mungu kedmon nyawaje wa KANISA la EAGT wokovu ndiyo Sasa ministries center iringa.0620620199