UKHTY MAI

UKHTY MAI page
hili ni wanawake tu

11/03/2024

PICHA CHAFU FACEBOOK.

Ndugu zangu, kumekuwa na muendelezo wa watu kuwa tagged na video za ngono kwenye mtandao wa Facebook kwa siku za karibuni. Jambo hili limezua sintofahamu miongoni mwa jamii.

Ili kuepuka kuwa tagged kwa video au picha chafu, fanya yafuatayo:

Ingia kwenye Settings ya Facebook Account yako kisha nenda Audience and Visibility halafu nenda Profile and Tagging.

Ukishafika hapo Profile and Tagging utakuta kuna machaguo mawili la kwanza linahusu Viewing and Sharing.

Kwenye 'Who can post on your profile' chagua 'Only Me' vivyo hivyo kwenye 'Who can see what others post on your profile' chagua 'Only Me.'

Pia, kwenye Tagging lile chaguo la kwanza lililoandikwa, 'Who can see posts you're tagged in on your profile' chagua 'Only Me'.

Aidha, pale kwenye option ya 'When you're tagged in a post, who do you want to add to the audience of the post if they can't already see it' napo chagua 'Only Me.'

Sharing is caring.
Mfahamishe na mwenzako.

🌻🌻FADHILA ZA MWEZI RAJABU NA YALIYOZULIWA NDANI YAKE⚘️⚘️Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hu...
30/01/2024

🌻🌻FADHILA ZA MWEZI RAJABU NA YALIYOZULIWA NDANI YAKE⚘️⚘️

Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo iko minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu, na piganeni vita na washirikina wote k**a wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]

Hapana shaka kutokana na Aayah hizo kwamba miezi hii minne mitukufu hutakiwa kutukuzwa inavyopaswa, kwa kutokufanya maasi na kudhulumiana, kwani malipo ya kufanya madhambi katika miezi hii mitukufu huwa ni makubwa zaidi. Katika kuiheshimu pia ni kumcha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) zaidi kwa kila aina ya 'ibaadah. Lakini sio kwa kuchagua siku maalumu ambazo watu wametenga kwa ajili ya kusherehekea na kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kutokana na kuaminika utukufu wa siku hizo au matukio yake ya kihistoria.

Baadhi ya mambo yanayotendeka katika mwezi huu ambayo hayana uthibitisho kutoka katika Qur-aan wala Sunnah:

Kuitukuza siku inayosemwa ni ya Mi’raaj au Israa na Mi’raaj (ambayo inadaiwa na wengi kuwa ilikuwa katika mwezi huu wa Rajab, na kudaiwa ni tarehe 27) kwa kufunga hasa siku hii pekee.

Baadhi ya watu wameanzisha Swalaah ambayo wameiita Swalaat Ar-Raghaaib, ambayo huswaliwa mwanzoni mwa mwezi huu. Hii ni k**a ile hali ya mwezi wa Sha'baan na haswa katikati yake ambayo watu wamezusha jina liitwalo Laylatul Baraa-ah (wakisema ni usiku wa ahadi na kusamehewa waliokufa au ni usiku wa kuwekwa mbali na madhambi) ambapo watu hufanya ni usiku wa 'ibaadah na kuswali sana na kufunga mchana wake.

Watu wametunga du'aa na aina ya Istighfaar na Adhkaar mbali mbali kuwa ni maalumu zisomwe katika mwezi huu wa Rajab.

Kuzuru makaburi.

Watu kujumuika na kufanya mihadhara na kupeana mawaidha ya kuelezana historia ya tukio la Israa na Mi'raaj.


Hizi ni sherehe na mipangilio ya 'ibaadah ambayo hayamo katika shariy'ah katu, na wala hazijathibiti katika ushahidi sahihi sehemu yoyote katika vyanzo vya kutegemewa. Ni mambo ya uzushi ambayo baaadhi ya watu wameyazusha kwa ajili ya kuzitukuza siku hizo kutokana na kudhani kufanya hivyo kutawapatia ujira na kuwaongezea daraja yao ya Dini.


Ukifanya utafiti na kupitia katika maandiko yenye kutegemewa, utakuta hakuna uthibitisho wa kusherehekea na kufanya 'ibaadah zozote maalum katika siku hiyo na usiku huo. Pia hakuna ushahidi sahihi wa kufunga Swawm katika siku hiyo ya tarehe 27 ya mwezi wa Rajab. K**a ambavyo hakuna kitu kiitwacho Laylatul Baraa-ah ambayo baadhi ya watu wameiita hiyo siku ya katikati au tarehe 15 ya mwezi wa Sha'baan, ambao ni usiku wa masiku yenye fadhila ambao Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((Allaah Anawatazama viumbe wake katika usiku wa kumi na tano wa Sha'baan na kisha huwasamehe ila wale washirikina au wale wenye kuwa na Uadui)) [Ibn Maajah]


Hakuna ushahidi na ukweli halisi wa kuwa usiku huo wa safari tukufu ya Nabiy wetu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya Israa na Mi'iraaj, kuwa ulikuwa ni katika siku hii ya tarehe 27 ya Rajab, na hata k**a ikisemwa kuwa ilikuwa ni siku hiyo na wasio na ushahidi, bado hakuna mafundisho yoyote yenye kutueleza kuwa tunapaswa kufunga katika siku hii. Bali tutakapofanya hivyo, tutakuwa tumezua jambo lililo nje ya shariy'ah. Hata hivyo, haikatazwi kwa mtu aliyezoea kufunga Jumatatu na Alkhamiys kufunga Swawm zake ikiwa zimeeangukia katika siku hii ya tarehe 27 ya Rajab, au Swawm ya masiku meupe au kulipa madeni yake n.k.


Na k**a kuna masiku yenye kushukuriwa na ambayo yamepaswa kukumbukwa kwake kwa kufunga Swawm, basi ni ile siku ya tarehe kumi ya mwezi Muharram au 'Aashuraa ambayo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaamrisha Maswahaba zake kuifunga kwa ajili ya kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kumuokoa Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) kutoka katika balaa la Fir'awn na jeshi lake. Na lisingekuwa jambo gumu au kushindikana kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutufundisha sisi au kutuamrisha kufunga katika siku hii ya 27 ya Rajab k**a angetaka, k**a alivyotuamrisha kufunga Swawm ya 'Aashuraa na siku kabla yake au baada yake. Lakini hakufanya hivyo! Na maadam hakutuelekeza kufanya hivyo, na yeye hakufanya hivyo, basi hakuna maana ya sisi kuwa mahodari na mafundi wa kujipangia mambo ambayo mbora wetu hakuyaonea umuhimu kwetu kuyafanya.

Ama ya kukusanyana katika siku hiyo ya tarehe 27 Rajab, kwa ajili ya kupeana mawaidha na kuelezana historia ya tukio hilo, ni bora liepukwe na ni vizuri kuwahimiza watu kuhudhuria madarsa Misikitini na mihadhara ili waweze kuyajua hayo na mengi mengine ambayo ni muhimu zaidi katika Dini yao. Kuwepo kwa minasabaat k**a hiyo ya kukusanyana kila linapotokea tukio, kunafungua milango ya uzushi na kuifanya Dini kuwa na mambo mengi na mazito hadi yale ya muhimu na yenye faida zaidi yakaachwa na kuendekezwa hayo ya mpito.

Leo hii tuna mifano mingi ya matukio sampuli hii k**a vile sherehe na mikusanyiko ya Mawlid, sherehe za nusu Sha'baan, sherehe za mwaka mpya wa Kiislam n.k.


Hata kwenye baadhi ya kalenda kumewekwa siku hizo k**a ni siku za sikukukuu. Na tunaona leo hii hata baadhi ya nchi zimeweka sikukuu rasmi ya Mawlid, na kuwapa Waislam mapumziko! Waislam wengi wamefurahi kuona kuwa 'wametambuliwa' na 'kuthaminiwa', ilhali mambo hayo hayana asli katika Dini.

10/06/2023

*𝗡I 𝗨𝗢𝗩𝗨 𝗔𝗖𝗛𝗔*✋

Jambo la kunasibisha ama kutambulisha tabia chafu za baadhi ya Watu kwa makabila yao ni jambo Ovu, Liepuke✋

Mara kadhaa nimesikia watu wakisema👇

👉𝗨𝘀𝗶𝗼𝗲 𝗮𝘂 𝗞𝘂𝗼𝗹𝗲𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗪𝗮𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗞𝗔𝗕𝗜𝗟𝗔 𝗹𝗶𝗹𝗲, 𝗻𝗶 𝗠𝗮𝗹𝗮𝘆𝗮 𝘀𝗮𝗻𝗮,

Au

👉𝗨𝘀𝗶𝗼𝗲 𝗮𝘂 𝗞𝘂𝗼𝗹𝗲𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗪𝗮𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗞𝗔𝗕𝗜𝗟𝗔 𝗹𝗶𝗹𝗲, 𝗻𝗶 𝗪𝗮𝘀𝗵𝗶𝗿𝗶𝗸𝗶𝗻𝗮 𝘀𝗮𝗻𝗮,

Au

👉𝗞𝗔𝗕𝗜𝗟𝗔 𝗹𝗶𝗹𝗲 𝗹𝗶𝗻𝗮𝘀𝗶𝗳𝗶𝗸𝗮 𝗸𝘄𝗮 𝗧𝗮𝗯𝗶𝗮 𝗖𝗵𝗮𝗳𝘂, 𝘂𝘀𝗶𝗲𝗻𝗱𝗲 𝗸𝘂𝗼𝗮 𝗽𝗮𝗹𝗲 𝗮𝘂 𝗸𝘂𝗼𝗹𝗲𝘄𝗮 𝗻𝗮𝗼.
___

Hayo maneno kutoka kwa vinywa vya watu wasio na hoja wala dalili nimeyasikia sana tu. Ama kwa hakika ni dhana potofu🚮 isiyo na hoja za kiakili wala dalili za Kimaandiko kuchafua Makabila ya wengine kwa Uchafu wa wachache wao.

➡️Hoja ya kusema, Watu wa Kabila fulani ni Malaya, je! Umechunguza kabila zima, maana kabila si kikundi cha watu watano au kumi bali kabila ni mjumuiko watu wengi.

➡️Hoja ya kusema, Kabila lile watu wake wamekithiri kwa Ushirikina, je! Umepata data za kila mtu ndani ya kabila hilo? Au je! umepata Elimu ya ghaibu kufahamu hata yale yaliyofichika kwa Watu?

Kwa kuchafua Makabila ya wengine kwa uchafu ufanywao na wachache wao, huo ni Uovu na ni kujiona kabila lako ni bora kuliko wengine (UKABILA). Na Mtume (صلى الله عليه وسلم) amekemea sana suala zima la Ukabila.

Jubair Ibn Mut'im رضي الله عنه aliarifu: Mtume wa Allah (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙎𝙞 𝙢𝙞𝙤𝙣𝙜𝙤𝙣𝙞 𝙢𝙬𝙚𝙩𝙪 𝙮𝙪𝙡𝙚 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙖𝙣𝙖𝙞𝙩𝙞𝙖 𝙐𝙠𝙖𝙗𝙞𝙡𝙖. 𝙎𝙞 𝙢𝙞𝙤𝙣𝙜𝙤𝙣𝙞 𝙢𝙬𝙚𝙩𝙪 𝙮𝙪𝙡𝙚 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙖𝙣𝙖𝙥𝙞𝙜𝙖𝙣𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙖𝙟𝙞𝙡𝙞 𝙮𝙖 𝙐𝙠𝙖𝙗𝙞𝙡𝙖. 𝙎𝙞 𝙢𝙞𝙤𝙣𝙜𝙤𝙣𝙞 𝙢𝙬𝙚𝙩𝙪 𝙮𝙪𝙡𝙚 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙠𝙖𝙛𝙖 (𝙞𝙡𝙝𝙖𝙡𝙞) 𝙖𝙠𝙞𝙛𝙪𝙖𝙩𝙖 𝙢𝙬𝙚𝙣𝙚𝙣𝙙𝙤 𝙬𝙖 𝙐𝙠𝙖𝙗𝙞𝙡𝙖."
((𝖲𝗎𝗇𝖺𝗇 𝖠𝖻𝗂 𝖣𝖺𝗐𝗎𝖽, 5121))
((𝖣𝖺𝗋𝖺𝗃𝖺: 𝖧𝖺𝗌𝖺𝗇))
____

𝖬𝗍𝗎 𝗆𝗐𝖾𝗇𝗒𝖾 𝖿𝗂𝗄𝗋𝖺 𝖺𝗎 𝗆𝗍𝖺𝗓𝖺𝗆𝗈 𝗐𝖺 𝖴𝗄𝖺𝖻𝗂𝗅𝖺 𝗇𝗂 𝗄𝖺𝗆𝖺 𝗆𝖿𝖺𝗇𝗈 𝗐𝖺 𝗇𝗀𝖺𝗆𝗂𝖺 𝖺𝗅𝗂𝗒𝖾𝗍𝗎𝗆𝖻𝗎𝗄𝗂𝖺 𝗄𝗂𝗌𝗂𝗆𝖺𝗇𝗂, 𝗄𝗂𝗌𝗁𝖺 𝖺𝗄𝖺𝖿𝖺 𝗇𝖺 𝗄𝗎𝗈𝗓𝖺, 𝗇𝖺 𝗆𝗐𝗂𝗌𝗁𝗈𝗐𝖾 𝗂𝗄𝖺𝗅𝖺𝗓𝗂𝗆𝗂𝗄𝖺 𝗄𝗎𝗏𝗎𝗍𝗐𝖺 𝗇𝗃𝖾 𝗒𝖺 𝗄𝗂𝗌𝗂𝗆𝖺 𝗄𝗐𝖺 𝗄𝗎𝗍𝗎𝗆𝗂𝖺 𝗆𝗄𝗂𝖺 𝗐𝖺𝗄𝖾.

Amesema Mtume wa Allah (صلى الله عليه وسلم)👇

"𝙈𝙛𝙖𝙣𝙤 𝙬𝙖 𝙢𝙩𝙪 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙖𝙣𝙖𝙪𝙣𝙜𝙖 𝙢𝙠𝙤𝙣𝙤 𝙬𝙖𝙩𝙪 𝙬𝙖𝙠𝙚 𝙥𝙖𝙨𝙞 𝙣𝙖 𝙝𝙖𝙠𝙞 (𝙪𝙠𝙬𝙚𝙡𝙞 𝙬𝙖 𝙟𝙖𝙢𝙗𝙤 𝙝𝙪𝙨𝙞𝙠𝙖) 𝙣𝙞 𝙠𝙖𝙢𝙖 𝙢𝙛𝙖𝙣𝙤 𝙬𝙖 𝙣𝙜𝙖𝙢𝙞𝙖 𝙢𝙛𝙪 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙠𝙖𝙩𝙪𝙢𝙗𝙪𝙠𝙞𝙖 𝙠𝙞𝙨𝙞𝙢𝙖𝙣𝙞 𝙣𝙖 𝙖𝙠𝙖𝙫𝙪𝙩𝙬𝙖 (𝙖𝙠𝙖𝙤𝙣𝙙𝙤𝙨𝙝𝙬𝙖) 𝙠𝙬𝙖 𝙠𝙪𝙩𝙪𝙢𝙞𝙖 𝙢𝙠𝙞𝙖 𝙬𝙖𝙠𝙚."
((𝘔𝘶𝘴𝘯𝘢𝘥 𝘈𝘩𝘮𝘢𝘥, 3670))
((𝘋𝘢𝘳𝘢𝘫𝘢: 𝘚𝘢𝘩𝘪𝘩))
____

Mtu ambaye ametumbukia kwenye dhambi hii ya Ukabila ameangamia, ndiyo k**a tu ngamia aliyetumbukia kwenye kisima hadi kifo chake kikamfika, kwa hakika Mzoga wake utatia sumu kisima cha mji mzima. Hii ina maana kwamba mwenye Ukabila huchafua taswira ya Kabila zima la wengineo huku akilipa usafi kabila lake. Huyu hana tofauti na mzoga wa ngamia uliofia kisimani na kuoza, na hauna budi kuondoshwa.

Si vyema watu au kikundi cha watu kujiona wao ni bora zaidi na wengine kuwaona waovu zaidi. Vivyo hivyo si vyema kuliona kabila lako ni bora zaidi kitabia huku ukichafua hadhi ya makabila mengineo kwa kuyanasibisha na tabia chafu na mbaya k**a Umalaya au Ushirikina.

Imepokewa kutoka kwa 'Aisha (رضي الله عنها) kwamba, Mtume wa Allah (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙈𝙪𝙤𝙫𝙪 𝙯𝙖𝙞𝙙𝙞 𝙢𝙞𝙤𝙣𝙜𝙤𝙣𝙞 𝙢𝙬𝙖 𝙬𝙖𝙩𝙪 𝙣𝙞 𝙢𝙩𝙪 𝙖𝙣𝙖𝙮𝙚𝙢𝙩𝙪𝙨𝙞 𝙢𝙩𝙪 𝙢𝙬𝙚𝙣𝙜𝙞𝙣𝙚 𝙝𝙪𝙠𝙪 𝙖𝙠𝙞𝙙𝙝𝙖𝙡𝙞𝙡𝙞𝙨𝙝𝙖 𝙆𝙖𝙗𝙞𝙡𝙖 𝙯𝙞𝙢𝙖; 𝙣𝙖 𝙢𝙩𝙪 𝙖𝙣𝙖𝙮𝙚𝙢𝙠𝙖𝙣𝙖 𝘽𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙖𝙠𝙚 𝙣𝙖 𝙠𝙪𝙢𝙨𝙝𝙪𝙩𝙪𝙢𝙪 𝙈𝙖𝙢𝙖 𝙮𝙖𝙠𝙚 𝙠𝙬𝙖 𝙐𝙯𝙞𝙣𝙯𝙞."
((𝘚𝘶𝘯𝘢𝘯 𝘐𝘣𝘯 𝘔𝘢𝘫𝘢𝘩, 3761))
((𝘒𝘐𝘵𝘢𝘣𝘶 𝘤𝘩𝘢 33, 𝘏𝘢𝘥𝘪𝘵𝘩 105))
((𝘋𝘢𝘳𝘢𝘫𝘢 𝘏𝘢𝘴𝘢𝘯/𝘋𝘢𝘳𝘶𝘴𝘚𝘢𝘭𝘢𝘢𝘮))
___

Katika Hadith nyingine, Mtume wa Allah (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙈𝙪𝙤𝙫𝙪 𝙯𝙖𝙞𝙙𝙞 𝙢𝙞𝙤𝙣𝙜𝙤𝙣𝙞 𝙢𝙬𝙖 𝙬𝙖𝙩𝙪 𝙣𝙞 𝙢𝙨𝙝𝙖𝙞𝙧𝙞 𝙖𝙢𝙗𝙖𝙮𝙚 𝙝𝙪𝙙𝙝𝙖𝙡𝙞𝙡𝙞𝙨𝙝𝙖 𝙠𝙖𝙗𝙞𝙡𝙖 𝙯𝙞𝙢𝙖."
((𝘈𝘭-𝘈𝘥𝘢𝘣 𝘢𝘭-𝘔𝘶𝘧𝘳𝘢𝘥, 870))
((𝘋𝘢𝘳𝘢𝘫𝘢: 𝘚𝘢𝘩𝘪𝘩))
____

Kwa mujibu wa hadithi hizo za Mtume صلى الله عليه وسلم, haifai Mtu kulichafua ama kulidhalilisha Kabila zima kwa Uchafu wa wachache miongoni mwao. Uislamu unakataza kujumuisha makosa ya wachache kwa jopo la walio wengine, yaani hairuhusiwi kuchafua kundi zima la watu kwa uchafu wa wachache wao. Kwa sababu watu wasio na hatia hawawezi kuwajibishwa kwa makosa ya wengineo. ALLAH TAALAH amesema ndani ya Qur'an👇

ۚ وَلَا تَكْسِبُ كُلُّ نَفْسٍ إِلَّا عَلَيْهَا ۚ وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُم مَّرْجِعُكُمْ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ فِيهِ تَخْتَلِفُونَ

(AL - AN-A'AM - 164)
"..Na kila nafsi haichumii ila nafsi yake. Na habebi mwenye kubeba mzigo wa mwenziwe. Kisha marejeo yenu ni kwa Mola wenu Mlezi, naye atakuambieni mliyo kuwa mkikhitalifiana."
____

Na katika Hadithi iliyopokelewa na Abdullah Ibn Mas'ud aliarifu: Mtume wa Allah (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙈𝙩𝙪 𝙖𝙨𝙞𝙖𝙙𝙝𝙞𝙗𝙞𝙬𝙚 𝙠𝙬𝙖 𝙢𝙖𝙠𝙤𝙨𝙖 𝙮𝙖 𝘽𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙖𝙠𝙚 𝙖𝙪 𝙣𝙙𝙪𝙜𝙪 𝙮𝙖𝙠𝙚."
((𝘚𝘶𝘯𝘢𝘯 𝘈𝘯-𝘯𝘢𝘴𝘢𝘪, 4131))
((𝘋𝘢𝘳𝘢𝘫𝘢: 𝘚𝘢𝘩𝘪𝘩))

Hapa tunajifunza kuwa si vyema kumuingiza mtu makosani kwa kosa alilolifanya mwengine eti kwa sababu tu ya Unasaba. Na vivyo hivyo, haifai kuliingiza kabila zima makosani kwa makosa yafanywayo na wachache ndani yake, watiwe makosani wao k**a wao.
______

𝗨𝗞𝗔𝗕𝗜𝗟𝗔 𝗡𝗔 𝗡𝗗𝗢𝗔

Hakuna Aya yoyote ile ndani ya Qur'an, wala hakuna Hadithi Sahih au dhaifu ambazo zimetaja kwamba, moja kati ya kigezo cha kuoa au kuolewa ni kutazama Kabila la mtu. Aya hiyo au hadithi hiyo hakuna. Bali vigezo alivyovitaja Mtume (صلى الله عليه وسلم) ni k**a vilivyoelezwa katika Hadithi zifauatazo👇

Abu Hurayrah (رضي الله عنه) ameeleza kuwa: Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙈𝙬𝙖𝙣𝙖𝙢𝙠𝙚 𝙖𝙣𝙖𝙤𝙡𝙚𝙬𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙫𝙞𝙩𝙪 𝙫𝙞𝙣𝙣𝙚: 𝙠𝙬𝙖 𝙪𝙩𝙖𝙟𝙞𝙧𝙞 𝙬𝙖𝙠𝙚, 𝙠𝙬𝙖 𝙪𝙟𝙪𝙯𝙞 𝙬𝙖𝙠𝙚, 𝙠𝙬𝙖 𝙪𝙯𝙪𝙧𝙞 𝙬𝙖𝙠𝙚 𝙣𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙙𝙞𝙣𝙞 𝙮𝙖𝙠𝙚. 𝙈𝙘𝙝𝙖𝙜𝙪𝙚 𝙮𝙪𝙡𝙚 𝙢𝙬𝙚𝙣𝙮𝙚 𝙢𝙨𝙞𝙢𝙖𝙢𝙤 𝙢𝙯𝙪𝙧𝙞 𝙬𝙖 𝘿𝙞𝙣𝙞."
((𝘉𝘶𝘬𝘩𝘢𝘳𝘪 𝘯𝘢 𝘔𝘶𝘴𝘭𝘪𝘮))

Kigezo kikuu ambacho Mtume (صلى الله عليه وسلم) amekipendekeza kwa Mwanamke kuolewa ni Msimamo mzuri wa Dini yake.

Katika hadithi nyingine, Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema👇

"𝙋𝙞𝙣𝙙𝙞 𝙖𝙣𝙖𝙥𝙤𝙠𝙪𝙟𝙞𝙚𝙣𝙞 𝙢𝙣𝙖𝙚𝙧𝙞𝙙𝙝𝙞𝙖 𝘿𝙞𝙣𝙞 𝙮𝙖𝙠𝙚 𝙣𝙖 𝙩𝙖𝙗𝙞𝙖 𝙮𝙖𝙠𝙚 𝙠𝙪𝙬𝙖 𝙣𝙞 𝙣𝙯𝙪𝙧𝙞, 𝙗𝙖𝙨𝙞 𝙢𝙪𝙤𝙯𝙚𝙨𝙝𝙚𝙣𝙞..𝙆𝙖𝙢𝙖 𝙝𝙪𝙩𝙖𝙛𝙖𝙣𝙮𝙖 𝙝𝙞𝙫𝙮𝙤 𝙥𝙖𝙩𝙖𝙠𝙪𝙬𝙖 𝙣𝙖 𝙝𝙪𝙯𝙪𝙣𝙞 (𝙢𝙖𝙩𝙖𝙩𝙞𝙯𝙤) 𝙣𝙖 𝙫𝙪𝙧𝙪𝙜𝙪 𝙠𝙖𝙩𝙞𝙠𝙖 𝙪𝙡𝙞𝙢𝙬𝙚𝙣𝙜𝙪."
___

Kwa hiyo hapa tunaona sifa za Mume zilizotajwa ni mbili tu, Dini na tabia yake njema. Hapo hakuna Sifa ya UKABILA ili Kuonesha kwamba Ukabila hauna nafasi katika UISLAMU.

Si Mbora wala Mwema kwa Ukabila au Utaifa wake, bali Mbora mbele ya ALLAH ni yule mwenye Kumcha Yeye tu👇

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّهِ أَتْقَاكُمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ

(AL H'UJURAAT - 13)
"Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu (mbora) zaidi kati yenu kwa Allah ni huyo aliye mchamngu zaidi katika nyinyi. Hakika Allah ni Mwenye kujua, Mwenye khabari."
___

Hakuna mbora kwa Kabila wala Taifa lake, bali aliye mbora ni yule mwenye Kumcha ALLAH TAALAH zaidi katika Waja wake.
___

HIVYO BASI, FIKRA AU MTAZAMO HASI AU CHANYA WA UKABILA HAUNA NAFASI KATIKA UISLAMU.

Tabia ya Umalaya, Ushirikina na kadhalika, Si alama au Nembo ya Kabila fulani, bali Tabia hizo ni matamanio ya wahusika wenyewe. Hata huyo anayekashifu Makabila ya watu kwa Umalaya, usikute na yeye pia ana machafu yake makubwa tu likiwemo na hilo pia.
____

𝙒𝘼𝙇𝙇𝘼𝙃𝙐 𝘼'𝙇𝘼𝙈

𝙉𝘼𝙈𝙐𝙊𝙈𝘽𝘼 𝘼𝙇𝙇𝘼𝙃 𝘼𝙏𝙐𝙊𝙉𝙂𝙊𝙕𝙀 𝙆𝘼𝙏𝙄𝙆𝘼 𝙐𝙏𝙄𝙄𝙁𝙐 𝙒𝘼𝙆𝙀, 𝘼𝙈𝙄𝙄𝙉
__________

07/06/2023

*Kusherehekea Siku Ya Kuzaliwa (Birthday) Inafaa?*

JIBU:

AlhamduliLLah, Waswalaatu Was-salaam 'alaa Rasuli-Llah صلى الله عليه وآله وسلم Amma ba'ad,



Tunamshukuru ndugu yetu kwa kuuliza swali hili muhimu ambalo lenye kuhusu jambo ambalo Waislamu wengi wanalitenda wakati jambo lenyewe halina msingi wa mafundisho ya dini, bali ni katika mambo ya kuigiza makafiri.

Amesema Allaah سبحانه وتعالى

((وَلَن تَرْضَى عَنكَ الْيَهُودُ وَلاَ النَّصَارَى حَتَّى تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمْ))

((Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao)) Al-Baqarah:120

Miongoni mwa mila zao makafiri ni hizo za kuwasha mishumaa na kupuliza, na kuweka muziki na kadhalika, yote hayo ni mafundisho ya baatil yasiyompasa Muislamu kuyafuata bali ni kufuata mwendo wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم pamoja na Wema Waliotangulia (Salaf Swaalih) ambao haijathibitika kuwa walikuwa wakishereheka siku zao za kuzaliwa abadan.

Kwa hiyo haifai kabisa kusherehekea kwa aina yeyote hata k**a ni kualika watoto wenzake kukusanyika kula na kunywa tu, kwani kufanya hivi itakuwa ni mafundisho kwa wengine kuwa jambo hili linafaa kwa vile eti halina muziki au hupulizi mishumaa. Na kusita kwako kufanya hivyo itakuwa ni mafundisho ya wenzako na kizazi chako kuendelea kujiepusha na mila hizi na kila atakayewacha kufanya kwa mafundisho yako basi utapata thawabu zako kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى .

*Na Allaah Anajua Zaidi.*

🛍️🛍️🛍️🛍️🛍️🛍️```STARA YA MWANAMKE```___________________*HIJABU SAHIHI INAYO KUBALIWA KATIKA UISLAMU NA SHERIA ZAKE*      ...
09/05/2023

🛍️🛍️🛍️🛍️🛍️🛍️
```STARA YA MWANAMKE```
___________________
*HIJABU SAHIHI INAYO KUBALIWA KATIKA UISLAMU NA SHERIA ZAKE*

🌹🍃🌹
Uislamu umemuwajibisha mwanamke kujistiri ili ikamilike heshma yake na Utambulike ustaarabu juu yake kutokana na Wasio Staarabika
Na katika hilo ALLAH akaandaa Adabu kali Kwa mwanamke asiye Jistiri kisawasawa k**a Alivyo Amrisha yeye ALLAH ndio mtume akasema
_Wanawake Wanaovaa Nguo Lakini Wako Uchi Wenye Vichwa Vya Manundu, Hawatoingia Jannah Wala Hawatasikia Harufu Yake_

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((صِنْفَانِ مِنْ أَهْلِ النَّارِ لَمْ أَرَهُمَا: قَوْمٌ مَعَهُمْ سِيَاطٌ كَأَذْنَابِ الْبَقَرِ يَضْرِبُونَ بِهَا النَّاسَ، وَنِسَاءٌ كَاسِيَاتٌ عَارِيَاتٌ مُمِيلاَتٌ مَائِلاَتٌ رُءُوسُهُنَّ كَأَسْنِمَةِ الْبُخْتِ الْمَائِلَةِ، لاَ يَدْخُلْنَ الْجَنَّةَ وَلاَ يَجِدْنَ رِيحَهَا، وَإِنَّ رِيحَهَا لَيُوجَدُ مِنْ مَسِيرَةِ كَذَا وَكَذَا)) مسلم
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله *وسلم ) amesema: ((Aina mbili za watu wa motoni sijawaonapo [hawapo katika zama zangu]: Watu walio na mijeledi mfano wa mikia ya ng’ombe wanawapiga watu kwa mijeledi hiyo [kwa dhulma], na kundi la pili ni wanawake waliovaa nguo na ilhali wako uchi, wakitembea kwa maringo huku wakiyanyonga mabega yao na wakiwafunza wengineo kutenda k**a hivyo, vichwa vyao (vimetuna ) ni k**a nundu za ngamia-bukhti wanaodemadema. Watu hawa Hawatoingia Jannah wala hawataisikia hata harufu yake, na kwa hakika harufu yake husikika umbali kadha wa kadhaa)).*
[Muslim]

Ngamia bukhti – ni aina ya ngamia wenye shingo ndefu. Na hapa wanakusudiwa wanawake wanao funga vitu nyuma ya vichwa vyao au juu anatumisha kichwa anaweka nundu k**a ya ngamia🐪 hawa Wamelaaniwa.

*MAFUNZO NA MWONGOZO WA HADITHI HII :*

1. Kuna Haramisho la kuwapiga watu kwa dhulma na tisho kwamba wanao fanya hayo hawatoingia Jannah bali wala hawatasikia harufu yake.

2. Haramisho kwa wanawake kutokuvaa vazi la Hijaab *Aliloamrisha Allaah (سبحانه وتعالى) lenye sitara na heshima. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):*

وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ ۚ
*_"Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao na wahifadhi tupu zao, na wala wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa yale yanayodhihirika. Na waangushe khimaar (shungi) zao mpaka vifuani mwao, na wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa kwa waume zao, au baba zao, au baba za waume wao, au wana wao wa kiume, au wana wa kiume wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kiume wa kaka zao, au wana wa kiume wa dada zao, au wanawake wao (wa Kiislamu), au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, au wafuasi wanaume wasio na matamanio ya jimai miongoni mwa wanaume au watoto ambao hawatambui kitu kuhusu sehemu za siri za wanawake. Na wala wasipige miguu yao yakajulikana yale wanayoyaficha katika mapambo yao."_* [An-Nuwr (24: 31)]

Na rejea Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى) katika Al-Ahzaab (33: 59).

3. Hadiyth imetoa pia onyo kali la mwenye kuasi kutokuingia Jannah na kutoisikia harufu yake.

4. Wanawake wengi hawatambui vazi khasa la Hijaab sahihi ya kisheria, hivyo Hujifunika kichwa na huku uso ukiwa wazi na mapambo, na nguo za mikono mifupi, au za kubana zinazodhirisha maumbile ya mwili wote na nyinginezo hata kuonekana mwili wake ndani, na zilizojazwa mapambo ya rangi na ming’aro. Mwanamke anapaswa ajifunze sharti la vazi la Hijaab kwamba;

*_MASHARTI YA VAZI LA MWANAKE NI_*

(i) Avae Jilbaab lisitiri kiwiliwili chote cha mwanamke, (pamoja na khilafu iliyopo kati ya wanachuoni kuhusu suala la uwajibu wa kuufunika uso na kutoufunika); Lakini kauli sahihi na yenye nguvu ni mwanamke kufunika mwili wake wote na uso ni lazima kufunikwa na wala sio khiari kwa mujibu wa aya na hadithi na vitendo vya wanawake wa Maswahaba vilionesha wazi Kufunika uso ni lazima. *(ndio maana mtume Akaruhusu Mwanamke kufunua Uso Akiwa Kwenye swala au akiwa Anatuf kwenye nyumba tukufu Makka hapo Atafunua Uso kwa sharti kuwe hakuna Wanaume wanao weza kumtazama, na k**a kuna wanaume afunike uso wake hata k**a anaswali)*

(ii) Jilbaab la mwanamke lisiwe na mapambo mapambo ya kuonekana wazi;

(iii) Kitambaa cha Jilbaab kinatakiwa kiwe kizito (kisioneshe vazi la ndani);

(iv) Jilbaab linatakiwa liwe pana (lisibane);

(v) Jilbaab halitakiwi kutiwa manukato hasa anapotoka ndani ya nyumba yake ;

(vi) Vazi la mwanamke halitakiwi lifanane na mavazi ya kiume k**a kanzu /leo wakaleta madera na mfano wake;

(vii) Jilbaab halitakiwi lifanane na mavazi ya makafiri mitindo ya kikafiri ni Haraam mwislamu kuuiga;

(viii) Jilbaab halitakiwi liwe ni katika mavazi ya fakhari hasa Unapotaka kutoka nalo nje .
👆🏽👆🏽👆🏽👆🏽👆🏽
*Hizo ni sharti ambazo ni lazima Zitimizwe Ili Vazi la Mwanamke wa kiislam liwe sahihi kinyume na hapo Anapata dhambi kutokanje Akiwa Hajajistiri inavyo takiwa*

5. Mwili wa mwanamke ni thamani ambayo inapasa kuhifadhiwa na kufichwa ili isipotee thamani yake. Mfano wake ni k**a lulu katika kombe ambayo imehifadhika humo.

6. Mwanamke ambaye havai vazi la Hijaab sahihi ya kisheria na anayejipamba na kudhihirisha mapambo yake mbele ya wasiokuwa mahram wake, huyu anakusanya madhambi mengi na laana za ALLAH

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu Wake wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Aayah hizi zinawahusu wanawake Waumini wengineo wote:

يَا نِسَاءَ النَّبِيِّ لَسْتُنَّ كَأَحَدٍ مِّنَ النِّسَاءِ ۚ إِنِ اتَّقَيْتُنَّ فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا ﴿٣٢﴾
*_"Enyi wake wa Nabiy! Nyinyi si k**a yeyote yule katika wanawake; mkiwa na taqwa, basi msilegeze kauli asije akaingiwa tamaa ambaye moyoni mwake mna maradhi na semeni kauli inayokubalika."_*

وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ ۖ وَأَقِمْنَ الصَّلَاةَ وَآتِينَ الزَّكَاةَ وَأَطِعْنَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴿٣٣﴾
*_"Na bakieni(kaeni) majumbani mwenu, na wala msionyeshe mapambo na uzuri wenu kwa ajinabi(waume wa kando) na kujishaua k**a zama za ujahili. Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah na mtiini Allaah na Rasuli Wake. Hakika Allaah Anataka Akuondosheeni maovu enyi ahli wa nyumba (ya Nabiy) na Akutakaseni mtakaso barabara."_*
[Al-Ahzaab (33: 32-33)]

7. Wenye majukumu juu ya wanawake; mume, baba, kaka n.k. wanapaswa kuwahimiza na kuhakikisha kuwa wanawake wao wanavaa vazi la Hijaab, kwani wasipofanya hivyo watakuja kuulizwa kuhusu jukumu na amana yao waliyopewa kuichunga.

8. Wanawake wasiovaa Hijaab wanadhania kwamba wako katika maendeleo na kuwadharau wanaovaa Hijaab, na ilhali ni kinyume chake, kwamba wanaovaa vazi la Hijaab wana hadhi zaidi kuliko wasiovaa mbele ya watu na zaidi mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى). Je, yupi aliyekuwa na heshima zaidi? Anayevaa Hijaab au wale wanaotumiliwa kwa picha za tupu zao katika biashara zao?

9. Makatazo kwa wanawake wanaovaa nguo za wazi mno maharusini kwa kisingizio kuwa wako mbele ya wanawake wenziwao. Hivyo, wanafikia kuvaa nguo za kudhihirisha sehemu za mwili na hali mipaka yake ni kuonyesha sehemu ambazo huwa wazi wanapokuwa wakifanya kazi za nyumba majumbani mwao k**a uso, nywele, shingo, mikono na miguu. Hivyo ni kwa sababu sehemu hizo pia ndio sehemu zinazovaliwa mapambo ya wanawake k**a herini, vidani, bangili, vikufu vya miguu.

*_"ALLAH AWAJALIE KUWA WAKE WEMA WENYE KUJITAMBUA"_*
🪵🪵🪵🪵🪵

29/04/2023

Nawaandikia tafsiri Yake

𝐄𝐰𝐞 𝐦𝐰𝐞𝐧𝐲𝐞𝐳𝐢𝐦𝐮𝐧𝐠𝐮 𝐡𝐚𝐤𝐢𝐤𝐚 𝐦𝐢𝐦𝐢 𝐧𝐚𝐤𝐮𝐭𝐚𝐤𝐚 𝐦𝐮𝐞𝐥𝐞𝐤𝐞𝐳𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐮𝐣𝐮𝐳𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐨,𝐧𝐚 𝐧𝐚𝐤𝐮𝐨𝐦𝐛𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐰𝐞𝐳𝐞𝐬𝐡𝐞 𝐤𝐰𝐚 𝐮𝐰𝐞𝐳𝐨 𝐰𝐚𝐤𝐨,𝐧𝐚 𝐧𝐚𝐤𝐮𝐨𝐦𝐛𝐚 𝐟𝐚𝐝𝐡𝐢𝐥𝐚 𝐳𝐚𝐤𝐨 𝐤𝐮𝐛𝐰𝐚,𝐡𝐚𝐤𝐢𝐤𝐚 𝐰𝐞𝐰𝐞 𝐮𝐧𝐚𝐰𝐞𝐳𝐚,𝐧𝐚𝐦𝐢 𝐬𝐢𝐰𝐞𝐳𝐢 𝐧𝐚𝐰𝐞 𝐮𝐧𝐚𝐣𝐮𝐚 𝐧𝐚𝐦𝐢 𝐬𝐢𝐣𝐮𝐢,𝐧𝐚𝐰𝐞 𝐧𝐢 𝐦𝐣𝐮𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐲𝐚𝐥𝐞 𝐲𝐚𝐥𝐢𝐨𝐟𝐢𝐜𝐡𝐢𝐤𝐚𝐧𝐚.𝐄𝐰𝐞 𝐦𝐰𝐞𝐧𝐲𝐞 𝐳𝐢𝐦𝐮𝐧𝐠𝐮 ,𝐢𝐰𝐚𝐩𝐨 𝐣𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐡𝐢𝐥𝐢 𝐤𝐮𝐭𝐨𝐤𝐚𝐧𝐚 𝐧𝐚 𝐮𝐣𝐮𝐳𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐨

(𝕛𝕒𝕞𝕓𝕠 𝕦𝕝𝕠𝕜𝕦𝕤𝕦𝕕𝕚𝕒)

𝐥𝐢𝐧𝐚 𝐤𝐡𝐞𝐫𝐢 𝐧𝐚 𝐦𝐢𝐦𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐝𝐢𝐧𝐢 𝐲𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐧𝐚 𝐦𝐚𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐲𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐧𝐚 𝐦𝐰𝐢𝐬𝐡𝐨 𝐰𝐚 𝐣𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐥𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐤𝐚𝐫𝐢𝐛𝐮 𝐚𝐮 𝐦𝐛𝐚𝐥𝐢
𝐛𝐚𝐬𝐢 𝐧𝐚𝐤𝐮𝐨𝐦𝐛𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐰𝐞𝐳𝐞𝐬𝐡𝐞 𝐧𝐢𝐥𝐢𝐩𝐚𝐭𝐞,𝐧𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐟𝐚𝐧𝐲𝐢𝐞 𝐰𝐞𝐩𝐞𝐬𝐢 𝐤𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐛𝐚𝐫𝐢𝐤𝐢,𝐧𝐚 𝐢𝐰𝐚𝐩𝐨 𝐮𝐧𝐚𝐣𝐮𝐚 𝐤𝐰𝐚𝐦𝐛𝐚 𝐣𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐡𝐢𝐥𝐢 𝐧𝐢 𝐥𝐚 𝐬𝐡𝐚𝐫𝐢 𝐤𝐰𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐝𝐢𝐧𝐢 𝐲𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐧𝐚 𝐦𝐚𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐲𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐧𝐚 𝐦𝐰𝐢𝐬𝐡𝐨 𝐰𝐚 𝐣𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐥𝐚𝐧𝐠𝐮 𝐤𝐚𝐫𝐢𝐛𝐮 𝐚𝐮 𝐦𝐛𝐚𝐥𝐢 𝐛𝐚𝐬𝐢 𝐥𝐢𝐞𝐩𝐢𝐬𝐡𝐞 𝐧𝐚 𝐦𝐢𝐦𝐢 𝐧𝐚𝐦𝐢 𝐧𝐢𝐞𝐩𝐮𝐬𝐡𝐞 𝐧𝐚𝐥𝐨, 𝐧𝐚 𝐧𝐢𝐩𝐚𝐧𝐠𝐞 𝐣𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐣𝐞𝐧𝐠𝐢𝐧𝐞 𝐥𝐞𝐧𝐲𝐞 𝐤𝐡𝐞𝐫𝐢 𝐧𝐚𝐦𝐢 𝐩𝐨𝐩𝐨𝐭𝐞 𝐥𝐢𝐥𝐢𝐩𝐨,𝐤𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐧𝐢𝐥𝐢𝐝𝐡𝐢𝐬𝐡𝐞 𝐤𝐰𝐚𝐥𝐨."

29/04/2023

Leo jamani nasisi waislamu tuelekezane kusali swala ya Istikhara (kutaka msaada kwa Allah)

Ukiwa na jambo unalotaka kulifanya kwa mfano
Labda umechumbiwa au jambo lolote mtake ushauri Allah atakujibu

Muda kuanzia saa sita usiku hadi saa kumi namoja fajiri

𝐝𝐮𝐚 𝐲𝐚 𝐬𝐰𝐚𝐥𝐚𝐭𝐮 𝐈𝐬𝐭𝐢𝐤𝐡𝐚𝐫𝐚

𝑎𝑙𝑙𝑎ℎ𝑢𝑚𝑚𝑎 𝐼𝑛𝑛𝑖 𝑎𝑠𝑡𝑎𝑘ℎ𝑖𝑦𝑟𝑢𝑘𝑎 𝑏𝑖𝑖𝑙𝑚𝑖𝑘𝑎 𝑤𝑎𝑎𝑑𝑡𝑎𝑞𝑑𝑖𝑟𝑢𝑘𝑎 𝑏𝑖𝑞𝑢𝑑𝑟𝑎𝑡𝑖𝑘𝑎 𝑤𝑎𝑎𝑠,𝑎𝑙𝑢𝑘𝑎 𝑚𝑖𝑛 𝑓𝑎𝑑ℎ𝑤𝑖𝑙𝑖𝑘𝑎 𝑙𝑎𝑎𝑑ℎ𝑤𝑖𝑚𝑖 𝑓𝑎𝑖𝑛𝑛𝑎𝑘𝑎 𝑡𝑎𝑞𝑑𝑖𝑟𝑢 𝑤𝑎𝑙𝑎𝑎 𝑎𝑞𝑑𝑖𝑟𝑢 𝑤𝑎𝑡𝑎𝑎𝑙𝑎𝑚𝑢 𝑤𝑎𝑙𝑎𝑎𝑎𝑙𝑎𝑚𝑢 𝑤𝑎𝑎𝑛𝑡𝑎 𝑎𝑎𝑙𝑙𝑎𝑎𝑚𝑢 𝑙𝑔ℎ𝑢𝑦𝑢𝑢𝑏𝑖
𝐴𝑙𝑙𝑎ℎ𝑢𝑚𝑚𝑎 𝐼𝑛 𝑘𝑢𝑛𝑡𝑎 𝑡𝑎𝑎𝑙𝑎𝑚𝑢 𝑎𝑛𝑛𝑎 ℎ𝑎𝑑ℎ𝑎𝑎 𝑙,𝑎𝑚𝑟𝑎

(𝐽𝐚𝐦𝐛𝐨 𝐮𝐥𝐨𝐤𝐮𝐬𝐮𝐝𝐢𝐚)

𝐦𝐟𝐚𝐧𝐨. 𝐘𝐚𝐚 𝐫𝐚𝐛𝐛𝐢 𝐧𝐚𝐤𝐮𝐨𝐦𝐛𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐨𝐧𝐞𝐬𝐡𝐞 𝐟𝐥𝐚𝐧𝐢 𝐛𝐢𝐧 𝐟𝐥𝐚𝐧𝐢 𝐚𝐧𝐚𝐟𝐚𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐦𝐮𝐦𝐞 𝐰𝐚𝐧𝐠𝐮
𝐚𝐮 𝐧𝐚𝐨𝐦𝐛𝐚 𝐮𝐧𝐢𝐨𝐧𝐞𝐬𝐡𝐞 𝐤𝐚𝐦𝐚 𝐩𝐞𝐬𝐚 𝐡𝐢𝐢 𝐧𝐢𝐰𝐞𝐤𝐞 𝐤𝐰𝐞𝐧𝐲𝐞 𝐡𝐢𝐢 𝐛𝐢𝐚𝐬𝐡𝐚𝐫𝐚
𝕜𝕚𝕤𝕙𝕒 𝕦𝕟𝕒𝕖𝕟𝕕𝕖𝕝𝕖𝕒

𝑘ℎ𝑎𝑦𝑟𝑢𝑙𝑖𝑖 𝑓𝑖𝑖 𝑑𝑖𝑖𝑛𝑖𝑖 𝑤𝑎𝑚𝑎𝑎𝑎𝑠ℎ𝑖𝑖 𝑤𝑎𝑎𝑎𝑞𝑖𝑏𝑎𝑡 𝑎𝑚𝑟𝑖𝑖
𝑎𝑎𝑗𝑖𝑙𝑖ℎ 𝑤𝑎𝑎𝑎𝑎𝑗𝑖𝑙𝑖ℎ𝑖
𝑓𝑎𝑞𝑑𝑖𝑟ℎ𝑢𝑙𝑖𝑖 𝑤𝑎𝑦𝑎𝑠𝑠𝑖𝑟ℎ𝑢 𝑙𝑖𝑖 𝑡ℎ𝑢𝑚𝑚𝑎 𝑏𝑎𝑟𝑖𝑘𝑙𝑖𝑖 𝑓𝑖𝑖ℎ𝑖
𝑤𝑎𝑖𝑛𝑘𝑢𝑛𝑡𝑎 𝑡𝑎𝑎𝑙𝑎𝑚𝑢 𝑎𝑛𝑛𝑎 ℎ𝑎𝑑ℎ𝑎𝑎 𝑙,𝑎𝑚𝑟𝑎 𝑠ℎ𝑎𝑟𝑟𝑢𝑙𝑖𝑓𝑖𝑖 𝑑𝑖𝑖𝑛𝑖 𝑤𝑎𝑚𝑎𝑎𝑠ℎ𝑖𝑖 𝑤𝑎𝑎𝑞𝑖𝑏𝑎𝑡𝑖 𝑎𝑚𝑟𝑖𝑖
𝑎𝑎𝑗𝑖𝑙𝑖ℎ𝑖 𝑤𝑎𝑎𝑎𝑗𝑖𝑙𝑖ℎ𝑖
𝑓𝑎𝑠𝑤𝑟𝑖𝑓𝑢ℎ𝑢 𝑎𝑎𝑛𝑛𝑖𝑦 𝑤𝑎𝑎𝑠𝑤𝑟𝑖 𝑓𝑛𝑖𝑦 𝑎𝑎𝑛ℎ𝑢 𝑤𝑎𝑞𝑑𝑖𝑟 𝑙𝑖𝑦𝑎 𝑙𝑘ℎ𝑎𝑖𝑟𝑎 ℎ𝑎𝑖𝑡ℎ𝑢 𝑘𝑎𝑎𝑛𝑎 𝑡ℎ𝑢𝑚𝑚𝑎 𝑎𝑟𝑑𝑤𝑖𝑛𝑖𝑦𝑏𝑖ℎ.

K**a hujaelewa inbox
Au nipigie 0683602356

Address

Buzuruga
Mwanza
0683602356

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UKHTY MAI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share