14/07/2026
π¨EXCLUSIVE KILICHOTOKEA LEO (USAJILI WA CHUGA BOY)ππΎππΎ:
Baada ya kambi ya timu ya taifa ya Tanzania ya U20 kuvunjwa pale TFF Center, kiongozi wa Fountain Gate alikwenda kumfuata Issa Abushiri βChuga Boyβ ili kuanza maandalizi ya mwisho ya safari yake ya kwenda Ubelgiji, baada ya klabu ya KAA Gent kulipia tiketi zote za ndege kwaajili ya majaribio.
Hata hivyo, mambo yamekuwa tofauti! Chuga Boy amegoma kuondoka na kiongozi huyo, akidai kuwa tayari ameshamalizana na Young Africans (Yanga SC) kwa makubaliano ya mkataba wa miaka mitatu (3).
Katika makubaliano hayo na Yanga, Chuga Boy anapewa Tsh. Milioni 90 k**a pesa ya usajili (Sign-on fee) na mshahara wa Tsh. Milioni 5 kwa mwezi.
Hatua inayofuata sasa ni mchezaji huyo kuandika barua rasmi ya kuomba kuondoka Fountain Gate, huku Yanga wakitakiwa kulipa Tsh. Milioni 100 k**a kipengele cha kuvunja mkataba wake (Release Clause).
Taarifa zinasema viongozi wa KAA Gent ya Ubelgiji hawajafurahishwa kabisa na namna kiongozi huyo wa Fountain Gate alivyoshindwa kusimamia makubaliano na mipango yote waliyoweka tangu mwanzo.
Mtu wa karibu na Chuga Boy (achana na pinned post yake ya pili), ambaye Yanga walimsafirisha kutoka Arusha hadi Dar es Salaam akiwa na nakala ya mkataba
Amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kumshawishi kijana huyo kubadili mawazo, licha ya kwamba awali alikuwa anataka kuondoka Fountain Gate kwa heshima na baraka zote kufanikisha kufanya majaribio