22/02/2024
Ukiwa mzazi unawajibu wa kumsaidia Mwanao kujenga netwok ya maisha ya baadaye. Usimtenganishe na Dunia kwa kuwa unaweza kumpa kila kitu.Dunia yako k**a Mzazi ni robo ya Dunia atakayowahitaji wenzake:
1. Lazima acheze na watoto wa mtaani kwake ata k**a hawana viatu. Viatu ni jambo la muda na kupita.
2.Unapompitia Shule hakikisha watoto anaosoma nao na wako mtaani kwako huwaachi, wabebe Wote urudi nao kwenye gari, Mafuta yanabakia yaleyale, hawa watakuwa ndugu zake wakati wewe haupo duniani.
3. Usijiskie vibaya kumsubiri dakika 10 rafiki yake anayekaribia kutoka darasani .Wao watamsubiri miaka 10
Kwenye maisha hapo baadaye.
4. Wajue kwa Majina kadri unavyoweza Marafiki zake, wajue progress yao, wakiwa wanaumwa Mpe nafasi akawasalimie, utamjengea Bond kubwa kwenye maisha yake ya ukubwani.
5. Akiingia Darasa jipya, awaangalie watoto wenzake wasio na uwezo mkubwa, awape vitabu vyake watumie kusoma badala ya kuacha vinaharibika Ndani, kuna siku akiwa na miaka 40 kuna mwenzake Ofisini atamuonyesha kitabu Chenye jina lake alichompa. Watu wasio na uwezo wanajua kutunza vitabu.
6. Mfundishe kujali watoto wenzake na akushirikishe changamoto zao. Kuna wengine wanahitaji msaada.
7. Usiogope wala kusita kuchukua hatua anapokueleza changamoto za mtoto mwenzake zilizo Ndani ya uwezo wako.
8. Once in a while, pita kwenye play ground yao. Waangalie ata kwa dakika 10 na kuwapongeza kwa Michezo yao. Watakukumbuka daima.
9. Wakumbushe watoto wote kuwa kila mmoja Ana nafasi ya maisha bora hapo baadaye, wawe watoto wema daima.
10.Akihama Shule, hakikisha anawaaga wenzake na Asiondoke tu ghafla hata k**a ni darasa la kwanza,hii ina kumbukumbu sana baadaye wakiwa watu wazima.
Kumbuka mtoto mwenye networks ni tajiri wa maisha.
Copy&Paste Kuna la kujifunza hapa✍🏻