15/01/2026
Mchezo wa Al Ahly SC vs Yanga SC siku ya Ijumaa utapigwa kwenye uwanja wa Borg El Arab uliopo Alexandria ikiwa ni mwendo wa masaa 2:30 mpaka 4 kutoka Cairo kwa usafiri wa Treni au Basi✍️
Mchezo wa mwisho Yanga kucheza uwanjani hapo walipoteza bao 2-1 dhidi ya Al Ahly kwa bao la 94’ la Abdallah El Said.
DONDOO MUHIMU
- Pitch yake (Eneo la kuchezea) ina urefu wa Mita 105 na upana wa Mita 70.
- Uwanja huu upo Kilomita 1.5 kutoka kituo cha Treni na upo kilomita 15 kutoka Alexandria mjini.
- Una uwezo wa kuingiza mashabiki 86,000 walioketi na una paa moja tu liliofunikwa (VIP)
- Upo Jangwani (Kwenye mkondo wa jangwa la Cairo - Alexandria)
- Ni uwanja ambao hautarajiwi kujaa kwa sababu mashabiki wa Alexandria sio waendaji uwanjani k**a wa Cairo.
- Ni uwanja wa Kisasa mno licha ya muonekano wake wa kizamani✍️ Una huduma zote za kisasa na za viwango vya juu…! Migahawa, maduka, vyoo na kila kitu ni kizuri✍️
- Zamani Zamalek na Ahly walipeleka sana mechi zao ngumu huko Ila kwa sasa unatazamwa k**a uwanja wa kawaida tu na wanapeleka mechi zao kwa ajili ya mashabiki wa Kaskazini mwa Misri✍️
- K**a vilivyo viwanja vingi vya Misri, uwanja huu umejengwa kwenye ubunifu na usimamizi wa jeshi la Misri✍️
- Ni uwanja wa pili kwa Ukubwa Misri (Nyuma ya Misr Stadium 90K) na ni wa pili kwa umaarufu baada ya Cairo International ✍️
- Upo karibu mno na Bahari ya Mediterrania.
Mwenyeji!? Mjumbe wa K**ati ya utendaji ya Yanga anaujua vyema tu kwani 2016 alikuwa na Yanga wakati wakicheza hapo na ndiye aliyelinda chumba cha Yanga!